Jumamosi , 28th Dec , 2019

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM, Bashiru Ally amesema chama hicho hakitatoa tisheti za bure kwa wanachama wake Uchaguzi Mkuu ujao, badala yake wanachama wajinunukie wenyewe

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM, Bashiru Ally.

Bashiru Ally ametoa kauli hiyo wakati akiwa mkoani Kagera ambapo amesema maelekezo hayo ni kutoka kwa Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa ambapo amesema wamejipanga kutumia gharama ndogo kwenye Uchaguzi ujao.

Bashiru Ally amesema kuwa "matarajio yangu uchaguzi ujao tutatumia pesa kidogo, na tumeshasema hatutanunua tisheti za kuwagaiwa wanachama wakati wa Uchaguzi"

"Hakuna cha burena kwakweli hakuna cha bure kama Makao Makuu wanachapisha tisheti kuwapa wanachama maanake wamewaomba kwa Matajiri" amesema Bashiru Ally